Skip to main content Skip to page footer

Diwani ya 'Mungu Hadanganywi na Hadithi Nyingine' yaingia fainali ya Safal Kiswahili Prize for African Literature

Washindi wa fainali watatangazwa katika hafla rasmi ya tuzo hiyo itakayofanyika Julai 3, 2025, jijini Dar es Salaam, Tanzania.

Bw Nuhu Zuberi Bakari

Bw Nuhu Zuberi Bakari (kati) akiwa na wanajopo wengine wakati wa uteuzi wa kutangaza miswada iliyoingia fainali. Picha/Hisani ya Safal

onyangoclara6@gmail.com

Mswada wa diwani ya ‘Mungu Hadanganywi na Hadithi Nyingine’ ulioandikwa na Mkenya Edwin Omindo umeorodheshwa miongoni mwa kazi bora zilizoingia fainali ya Safal Kiswahili Prize for African Literature kwa mwaka 2024.

Tuzo hiyo inadhaminiwa na The Safal Group kupitia kampuni ya Mabati Rolling Mills (MRM), na ilianzishwa mwaka 2014 na Dkt Lizzy Attere na Prof Mukoma wa Ngugi kwa lengo la kuenzi uandishi katika lugha za Kiafrika na kuhimiza tafsiri kutoka, kati ya, na kwenda kwenye lugha hizo.

Kwa mwaka huu, miswada 210 iliwasilishwa na kufanyiwa mapitio na jopo la majaji kabla ya kuchaguliwa kwa walioteuliwa kuingia fainali.

Miongoni mwa miswada iliyoingia fainali ni:

Mungu Hadanganywi na Hadithi Nyingine – Edwin Omindo (Kenya)

Nderemo za Mtaa – Joel Hamisi (Tanzania)

Kitanzi cha Mauti – Mayassa Abdallah Chembea (Tanzania)

Nyaraka za Wafu – Ali Othman Masoud (Tanzania)

Waadhi – Mohamed Hamid Haji (Tanzania)

Bure Ghali – Bashiru Abdallah (Tanzania)

Laana ya Uovu – Mohamed Idrisa (Tanzania)

Mwalimu Abdilatif Abdalla, Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa tuzo hiyo, alisema, “Inafurahisha sana kuona kuwa tangu mashindano yaanze mwaka 2015, Safal Prize imeendelea kuvutia idadi kubwa ya washiriki kutoka nchi mbalimbali. Ubora wa miswada pia umeongezeka kila mwaka, jambo ambalo linaendelea kuitajirisha fasihi ya Kiswahili.”

Washindi wa fainali watatangazwa katika hafla rasmi ya tuzo hiyo itakayofanyika Julai 3, 2025, jijini Dar es Salaam, Tanzania.

Jumla ya dola 15,000 za Kimarekani zitatolewa kwa miswada bora ambayo haijachapishwa katika vitengo vya riwaya, ushairi, wasifu, tamthilia, na riwaya za picha (graphic novels).

Miswada inayoshinda huchapishwa na Mkuki na Nyota Publishers wa Tanzania, huku mshindi wa ushairi akitafsiriwa kwa Kiingereza na kuchapishwa na Africa Poetry Book Fund.

Kwa mujibu wa Anthony Ng’ang’a, mmoja wa wadhamini wa Safal Kiswahili Prize:

“Tuzo hii ni zaidi ya kutambua vipaji vya fasihi – ni alama ya kuendeleza utambulisho wa Mwafrika. Kwa kuunga mkono kazi asilia katika Kiswahili, tunalinda na kuinua lugha inayowaunganisha, kuwahamasisha na kuwawezesha mamilioni ya watu barani Afrika.”

1573 results:
Raila takes holiday abroad, sparks debate online  
Date: 2025-08-24
Raila Odinga His retreat, though brief, arrives at a moment when speculation on succession politics and strategic maneuvering is high.  
End of the road for East Africa as hosts crash out of CHAN 2024  
Date: 2025-08-24
Senegal's Seyni Ndiaye shoots the ball past Ugandan player during their CHAN 2024 quarter-final match The East African dream is over--at least for now--and the Pamoja nations are left with memories of vibrant crowds, carnival atmospheres, and fleeting hope.  
Kenya vs Madagascar: Harambee Stars bow out of CHAN after penalty nightmare  
Date: 2025-08-23
Kenya Squad The match remained deadlocked through extra time, prompting a dramatic penalty shootout.  
East Africa’s hopes rest on Uganda as Kenya and Tanzania crash out of CHAN  
Date: 2025-08-23
Uganda Cranes The Cranes face Senegal in Kampala on Saturday (today) for a place in the last four(4).  
UoN pharmacy alumni mark golden jubilee with free medical camp  
Date: 2025-08-23
golden jubilee medical camp During the medical camp event, the Pharmaceutical Society of Kenya (PSK) raised alarm over rising cases of unqualified individuals infiltrating pharmacies.  
CHAN Quarter-Finals Set: Stakes high for hosts and challengers alike  
Date: 2025-08-22
Benni McCarthy Kenya, who topped Group A with 10 points, are under intense pressure to deliver in front of their home fans and reach the semi-finals for the first time.  
Speaker Wetang'ula warns MPs against corruption, absenteeism  
Date: 2025-08-21
Moses Wetang'ula The Speaker addressed claims of legislators soliciting inducements to influence legislation.  
Gachagua returns from a six-week US tour amid chaos at Kamukunji rally  
Date: 2025-08-21
Rigathi Gachagua The turbulence marked a dramatic contrast to the peaceful and symbolic nature of his US mission.  
High Court halts Ruto’s anti-corruption taskforce  
Date: 2025-08-21
The orders follow a petition filed by Nakuru-based surgeon Dr Magare Gikenyi, alongside Eliud Karanja Matindi, Philemon Abuga Nyakundi, and Dishon Keroti Mogire.  
Senate to hear governor Mutai's impeachment in plenary next week  
Date: 2025-08-20
Eric Mutai The Senate will handle the impeachment in a full House session, in line with Section 33A of the County Governments Act and Senate Standing Order 81B(2).  
Search results 1 until 10 of 1573