Skip to main content Skip to page footer

Kazi: Vijana walioasi mihadarati walia kubaguliwa

• Waraibu wa zamani wa dawa za kulevya wadai waajiri wengi - ikiwemo serikali ya kitaifa, kaunti na hata wanajamii wenyewe, wamekuwa wakiwabagua na kuwasuta.

Mwanamume apokea methadone kumsaidia kujinasua kutoka kwa uraibu wa mihadarati. Picha/AVDelta News

Afisa Msimamizi wa Waraibu na Matibabu katika Kituo cha Methadone cha King Fahd, Bw Juma Mwamvyoga. Picha/AVDelta News

Vijana waliojinasua kutoka kwa uraibu wa mihadarati kisiwani Lamu wanaililia serikali ya kitaifa na ile ya kaunti kuwapa kazi.

Vijana hao walidai kuwa kwa sasa wamebadilika kabisa, hasa kimkondo wa maisha na kwamba ni vyema ikiwa wataaminiwa na kupewa ajira.

Tena kilio chao ni kuwa kutokana na tabia chwara walizotambulika kuwa nazo, waajiri wengi - ikiwemo serikali ya kitaifa, kaunti na hata wanajamii wenyewe, wamekuwa wakiwabagua na kuwasuta.

Hii ni licha ya wao kuasi tabia mbaya.

Wakiongozwa na msemaji wao, Bw Shee Babli, ‘mateja’ hao wa zamani walishukuru mpango uliozinduliwa na serikali ya kaunti ya Lamu wa kuwapokeza matibabu waraibu hao wa mihadarati kupitia unywaji wa dawa aina ya methadone.

Vituo viwili vya methadone vimefunguliwa Lamu ambapo kufikia sasa tayari zaidi ya waraibu 400 wamefaulu kujinasua kutoka kwa janga hilo la mihadarati, hasa matumizi ya kokeni na heroni. Vituo hivyo ni King Fahd kisiwani Lamu na kile cha hospitali ya kisiwa cha Faza.

Bw Babli alisema licha ya kuweza kupokea mafunzo, kutibiwa kupitia methadone na kubadili maisha yao, tatizo kubwa linalowakumba wale wanaopona ni ukosefu wa ajira.

“Waajiri wengi bado wanatuona sisi kuwa wale wale mateja wa zamani, hivyo huwa hawataki ama tuwakaribie au kuwaomba kazi. Ni muhimu wafahamu Bw Babli wa sasa si yule wa miaka mitano iliyopita. Wengi wetu kwa sasa tumebadilika na msitubague. Sisi tumekuwa raia wema. Tupeni hizo ajira na tutatunza majukumu yetu vyema,” akasema Bw Babli.

Bw Athman Khamis, ambaye alikuwa mraibu wa mihadarati kwa zaidi ya miaka 10 na kisha kufaulu kujiokoa kutoka kwa janga hilo, alisema ukosefu wa ajira huenda ukawasukuma kurejelea maisha yao mabaya waliyoyapungia mkono wa kwaheri.

Alisema tayari ameshuhudia baadhi vya marafiki wake waliokuwa wameacha dawa za kulevya wakirudi kwenye uraibu kufuatia msongo wa mawazo uliosababishwa na wao kukosa ajira ili kujikimu kimaisha.

“Huku kuzurura ovyo mitaani kwa kukosa ajira ni kitu kibaya. Kumewasukuma wengi ambao walikuwa wameacha mihadarati kurejelea maisha hayo mabovu. Kaunti na serikali kuu ituonee imani. Watuamini na kutupa hizo ajira hata kama ni zile za kufagia mitaani ili tujukumike,” akasema Bw Athman.

Kauli ya vijana hao iliungwa mkono na Afisa Msimamizi wa Waraibu na Matibabu katika Kituo cha Methadone cha King Fahd, Bw Juma Mwamvyoga, aliyesema karibu asilimia 45 ya wale wanaopokea matibabu ya methadone wanaweza kuaminika, kupewa majukumu na kuyatekeleza vyema.

Bw Mwamvyoga alisema idara yake imesajili jumla ya waraibu wa mihadarati 712 kisiwani Lamu, ambapo wale ambao wamekuwa na bidii ya kupokea ushauri na kutumia methadone mfululizo tena inavyotakikana ni karibu 400.

“Ombi langu kwa serikali, wadau na mashirika ni kwamba ipo haja kuwaamini hawa vijana wanaopona kutoka kwa uraibu wa dawa za kulevya. Niko na karibu vijana 400 wanaotumia vyema methadone na wameonyesha kabisa mwelekeo bora wa maisha yao kubadilika kwa uzuri,” akasema Bw Mwamvyoga.

1573 results:
Raila takes holiday abroad, sparks debate online  
Date: 2025-08-24
Raila Odinga His retreat, though brief, arrives at a moment when speculation on succession politics and strategic maneuvering is high.  
End of the road for East Africa as hosts crash out of CHAN 2024  
Date: 2025-08-24
Senegal's Seyni Ndiaye shoots the ball past Ugandan player during their CHAN 2024 quarter-final match The East African dream is over--at least for now--and the Pamoja nations are left with memories of vibrant crowds, carnival atmospheres, and fleeting hope.  
Kenya vs Madagascar: Harambee Stars bow out of CHAN after penalty nightmare  
Date: 2025-08-23
Kenya Squad The match remained deadlocked through extra time, prompting a dramatic penalty shootout.  
East Africa’s hopes rest on Uganda as Kenya and Tanzania crash out of CHAN  
Date: 2025-08-23
Uganda Cranes The Cranes face Senegal in Kampala on Saturday (today) for a place in the last four(4).  
UoN pharmacy alumni mark golden jubilee with free medical camp  
Date: 2025-08-23
golden jubilee medical camp During the medical camp event, the Pharmaceutical Society of Kenya (PSK) raised alarm over rising cases of unqualified individuals infiltrating pharmacies.  
CHAN Quarter-Finals Set: Stakes high for hosts and challengers alike  
Date: 2025-08-22
Benni McCarthy Kenya, who topped Group A with 10 points, are under intense pressure to deliver in front of their home fans and reach the semi-finals for the first time.  
Speaker Wetang'ula warns MPs against corruption, absenteeism  
Date: 2025-08-21
Moses Wetang'ula The Speaker addressed claims of legislators soliciting inducements to influence legislation.  
Gachagua returns from a six-week US tour amid chaos at Kamukunji rally  
Date: 2025-08-21
Rigathi Gachagua The turbulence marked a dramatic contrast to the peaceful and symbolic nature of his US mission.  
High Court halts Ruto’s anti-corruption taskforce  
Date: 2025-08-21
The orders follow a petition filed by Nakuru-based surgeon Dr Magare Gikenyi, alongside Eliud Karanja Matindi, Philemon Abuga Nyakundi, and Dishon Keroti Mogire.  
Senate to hear governor Mutai's impeachment in plenary next week  
Date: 2025-08-20
Eric Mutai The Senate will handle the impeachment in a full House session, in line with Section 33A of the County Governments Act and Senate Standing Order 81B(2).  
Search results 1 until 10 of 1573