Skip to main content Skip to page footer

Buriani Mary Sinaida: Mwanzilishi wa Jerusaleum of Christ Church azikwa Kawangware

Kwenye mazishi hayo, wanasiasa kutoka mrengo wa ODM walifika kufariji waumini na familia.

Dorcus Mary Sinaida Akatsa

Dorcus Mary Sinaida Akatsa alizikwa mtaani Kawangware. Picha/Sancia Kagoni

Mwanzilishi wa Kanisa la Jerusaleum of Christ Church ‘Nabii’ Dorcus Mary Sinaida Akatsa alizikwa mtaani Kawangware mnamo Jumamosi.

Akatsa alipata heshima ya mwisho kutoka kwa waumini wake na wanasiasa mbalimbali ambao walihudhuria.

Waumini ambao walitajwa kuwa walipata nafasi za kazi katika idara ya kutoa huduma za usalama, walimpa heshima ya mwisho kwa kupiga gwaride na kumpigia saluti.

Miongoni mwa maafisa hao ni Veronica Marachi ambaye alimshukuru kiongozi huyo ambaye aliwezesha familia yake kupata makao mapya eneo la magharibi mwa Kenya.

“Asante kwa Mami. Alitununulia shamaba wakati wazazi wangu walikuwa wakichekwa na majirani. Hivi sasa ninayo kazi kutokana na maombi yake,” alikamilisha Bi Marachi.

Kwenye mazishi hayo, wanasiasa kutoka mrengo wa ODM walifika kufariji waumini na familia.

Viongozi hao wakiongozwa na Gavana wa Mombasa Abdullswamad Sheriff Nassir, seneta wa Nairobi Edwin Sifuna na Seneta wa Vihiga Godfrey Ososti.

Viongozi hao walitaja kuwa kuzikwa kwa mwili wa marehemu katika shamba hilo liliko mtaani Kawangware ni kulinda shamba hilo ambalo pia lilikuwa likimezewa na watu fulani.

Seneta Sifuna alisema atazidi kuungana na wana wa Akatsa--David Jogoo na Moses Sangolo--kuhakikisha mali yake hainyakuliwi.

Alidokeza kuwa alikutana na nabii huyo kabla ya kuchanguliwa kuwa Seneta wa Nairobi huku akiwa naye ataweza kupambana na wanyakuzi hao.

“Alinitembelea kwenye afisi yangu akaniombea na kunielezea matatizo yake. Alihakikisha tiketi yangu ya ndege ya kusafiri kutoka Nairobi hadi Kakamega inapatika kila wakati. Hadi pale nilifanikiwa kuweka mambo sawa,” alisema Bw Sifuna.

Kiongozi huyo aliwataka waumini kutafuta kiongozi mwingine ambaye atavalia kiatu cha nabii huyo ili kuunganisha waumini hao.

“Mungu amechukua yule amekuwa akifikisha dua zetu za maombi kwa Mungu. Hivi sasa tunaomba Mungu atupee nabii mwingine,” alikamilisha Bw Sifuna.

Aliyekuwa mwakilishi wa Wadi ya Gatina, Bw David Ayoi alisema kuwa awali kulikuwa na walaghai ambao walitaka kumnyanganya nabii huyo shamba la Kawangware 56 ambalo alijenga kanisa la Jerusaleum of Christ Church.

Kiongozi huyo akisistiza mwili wa nabii huyo kuzikwa katika eneo hilo litapunguzia tamaa kwa wale wanaotaka kuliiba.

Bw Ayoi alinishika mkono bw Ayoi wanataka kuninyanganya shamba langu, wameninyanganya zingine huko nyumbani. Walizikizana kila kitu na hivyo akalipia kila kitu na kushughulikia.

“Hili shamaba ambalo wanateea mate, tutazika mama hapa ili ijulikane shamba ni la mama. Tutashika watoto wake mkono na kanisa liendelee,” alikamilisha Bw Ayoi.

Mary Sinaida Akatsa almaarufu kama Dada Mary au Mami, alizaliwa mwaka wa 1964 huko Bunyore. 

Kulingana na familia yake, Akatsa alianza shule mwaka wa 1967 lakini aliacha masomo akiwa Darasa la Sita katika Shule ya Msingi ya Etabalia. 

Aliolewa na marehemu Francis Akatsa na ameacha wana wawili, David Jogoo na Moses Sangolo.

1573 results:
Raila takes holiday abroad, sparks debate online  
Date: 2025-08-24
Raila Odinga His retreat, though brief, arrives at a moment when speculation on succession politics and strategic maneuvering is high.  
End of the road for East Africa as hosts crash out of CHAN 2024  
Date: 2025-08-24
Senegal's Seyni Ndiaye shoots the ball past Ugandan player during their CHAN 2024 quarter-final match The East African dream is over--at least for now--and the Pamoja nations are left with memories of vibrant crowds, carnival atmospheres, and fleeting hope.  
Kenya vs Madagascar: Harambee Stars bow out of CHAN after penalty nightmare  
Date: 2025-08-23
Kenya Squad The match remained deadlocked through extra time, prompting a dramatic penalty shootout.  
East Africa’s hopes rest on Uganda as Kenya and Tanzania crash out of CHAN  
Date: 2025-08-23
Uganda Cranes The Cranes face Senegal in Kampala on Saturday (today) for a place in the last four(4).  
UoN pharmacy alumni mark golden jubilee with free medical camp  
Date: 2025-08-23
golden jubilee medical camp During the medical camp event, the Pharmaceutical Society of Kenya (PSK) raised alarm over rising cases of unqualified individuals infiltrating pharmacies.  
CHAN Quarter-Finals Set: Stakes high for hosts and challengers alike  
Date: 2025-08-22
Benni McCarthy Kenya, who topped Group A with 10 points, are under intense pressure to deliver in front of their home fans and reach the semi-finals for the first time.  
Speaker Wetang'ula warns MPs against corruption, absenteeism  
Date: 2025-08-21
Moses Wetang'ula The Speaker addressed claims of legislators soliciting inducements to influence legislation.  
Gachagua returns from a six-week US tour amid chaos at Kamukunji rally  
Date: 2025-08-21
Rigathi Gachagua The turbulence marked a dramatic contrast to the peaceful and symbolic nature of his US mission.  
High Court halts Ruto’s anti-corruption taskforce  
Date: 2025-08-21
The orders follow a petition filed by Nakuru-based surgeon Dr Magare Gikenyi, alongside Eliud Karanja Matindi, Philemon Abuga Nyakundi, and Dishon Keroti Mogire.  
Senate to hear governor Mutai's impeachment in plenary next week  
Date: 2025-08-20
Eric Mutai The Senate will handle the impeachment in a full House session, in line with Section 33A of the County Governments Act and Senate Standing Order 81B(2).  
Search results 1 until 10 of 1573