Skip to main content Skip to page footer

Mkenya Edwin Omindo anyakua Tuzo ya Safal ya Fasihi ya Kiswahili

Bw Edwin Omindo ni mwalimu wa shule ya msingi kutoka Luanda katika Kaunti ya Vihiga.

Mwalimu na Mwandishi Edwin Omindo

Mwalimu na Mwandishi Edwin Omindo. Picha/Hisani

Kwa miaka mingi, mashindano ya fasihi hujulikana kwa majina makubwa kutoka Tanzania, lakini mwaka huu wa 2025, katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, jina moja kutoka Kenya liliibua shangwe na nderemo.

Hakuwa mwingine bali Edwin Omindo, mwalimu wa shule ya msingi kutoka Luanda katika Kaunti ya Vihiga.

Bw Omindo mnamo Alhamisi alitunukiwa dola 5,000 (sawa na Sh650,000) kwa muswada wake wa hadithi fupi wenye kichwa kisicho cha kawaida na ambacho ni ‘Mungu Hadanganywi na Hadithi Nyingine’.

Usogora wake huo ndio uliomtambulisha si tu kama mshindi, bali kama mwandishi mwenye ucheshi, undani na ujasiri wa kuvuta msomaji kuanzia kichwa cha hadithi.

Katika orodha ya fainali ya Tuzo ya Safal ya Fasihi ya Kiswahili kwa mwaka 2024, Bw Omindo alikuwa ndiye Mkenya pekee, miongoni mwa majina saba yaliyoteuliwa kutoka mamia ya miswada iliyoletwa kutoka Afrika Mashariki.

Muswada wake ulishindana na kazi nyingine kutoka Tanzania. Kazi hizo ni pamoja na muswada wa ‘Kitanzi cha Mauti’ wake Mayasa Abdalla Chembea, ‘Bure Ghali’ wa Bashiru Abdallah, ‘Nderemo za Mtaa’, ‘Waadhi’, ‘Laana ya Uovu’ na 'Nyaraka za Wafu". Hata hivyo, Bw Omindo aling’aa katika kipengele cha hadithi fupi--na akaipa Kenya heshima ya kipekee.

Kwa upande wa Tanzania, Mayasa Abdalla na Bashiru Abdallah waliibuka washindi katika vipengele vya riwaya na ushairi mtawalia, kila mmoja akituzwa dola 5,000 (Tshs milioni 13).

Katika hotuba ya pongezi, Afisa Mtendaji Mkuu wa ALAF Tanzania, Ashish Mistry, alisifu mchango wa Bw Omindo kwa kusema: “Kushinda kwake ni ishara kuwa vipaji haviko tu mijini au kwenye majukwaa ya kitaaluma--vipo hata mashinani, ndani ya madarasa ya shule za msingi.”

Mashindano haya yaliyoanzishwa mwaka 2014 na Dkt Lizzy Attree pamoja na Prof Mukoma wa Ngugi, hutoa jukwaa kwa waandishi wanaotumia lugha ya Kiswahili --lugha inayozidi kuenea, kubeba utambulisho, na kuunganisha watu wa tabaka zote.

Mwenyekiti wa Bodi ya Tuzo, Mwalimu Abdilatif Abdalla, alisisitiza kuwa kiwango cha ubora wa kazi zinazowasilishwa huimarika kila mwaka.

“Kuna mwamko wa kipekee wa ubunifu na umahiri miongoni mwa waandishi wanaojitokeza. Kiswahili sasa ni chombo cha fasihi za kisasa zenye uzito.”

Majaji, wakiongozwa na Dkt Salma Hamad, walikiri kuwa mwaka huu walipokea miswada iliyosheheni ubunifu, uhalisia wa maisha ya Kiafrika, na matumizi fasaha ya lugha.

Miswada inayoshinda huchapishwa na Mkuki na Nyota Publishers nchini Tanzania, hatua inayowahakikishia waandishi hao nafasi ya kuingia sokoni na kufikia wasomaji halisi.

Katika hafla hiyo ya Alhamisi, waliokuwepo walijumuisha viongozi wa serikali ya Tanzania, wakuu wa mikoa, wanataaluma, wanafunzi, wachapishaji, pamoja na wadau wa lugha na fasihi kutoka mataifa jirani.

Na kwa Edwin Omindo, mwalimu mnyenyekevu kutoka kijijini, huu ulikuwa ushindi wa roho, si tu kalamu.

Amedhihirisha kuwa si lazima uandike kutoka studio yenye kiyoyozi au maktaba ya kifahari ili kusikika barani Afrika.

Naam, Mungu hadanganywi. Na fasihi njema nayo haiwezi kufichwa.

1573 results:
Raila takes holiday abroad, sparks debate online  
Date: 2025-08-24
Raila Odinga His retreat, though brief, arrives at a moment when speculation on succession politics and strategic maneuvering is high.  
End of the road for East Africa as hosts crash out of CHAN 2024  
Date: 2025-08-24
Senegal's Seyni Ndiaye shoots the ball past Ugandan player during their CHAN 2024 quarter-final match The East African dream is over--at least for now--and the Pamoja nations are left with memories of vibrant crowds, carnival atmospheres, and fleeting hope.  
Kenya vs Madagascar: Harambee Stars bow out of CHAN after penalty nightmare  
Date: 2025-08-23
Kenya Squad The match remained deadlocked through extra time, prompting a dramatic penalty shootout.  
East Africa’s hopes rest on Uganda as Kenya and Tanzania crash out of CHAN  
Date: 2025-08-23
Uganda Cranes The Cranes face Senegal in Kampala on Saturday (today) for a place in the last four(4).  
UoN pharmacy alumni mark golden jubilee with free medical camp  
Date: 2025-08-23
golden jubilee medical camp During the medical camp event, the Pharmaceutical Society of Kenya (PSK) raised alarm over rising cases of unqualified individuals infiltrating pharmacies.  
CHAN Quarter-Finals Set: Stakes high for hosts and challengers alike  
Date: 2025-08-22
Benni McCarthy Kenya, who topped Group A with 10 points, are under intense pressure to deliver in front of their home fans and reach the semi-finals for the first time.  
Speaker Wetang'ula warns MPs against corruption, absenteeism  
Date: 2025-08-21
Moses Wetang'ula The Speaker addressed claims of legislators soliciting inducements to influence legislation.  
Gachagua returns from a six-week US tour amid chaos at Kamukunji rally  
Date: 2025-08-21
Rigathi Gachagua The turbulence marked a dramatic contrast to the peaceful and symbolic nature of his US mission.  
High Court halts Ruto’s anti-corruption taskforce  
Date: 2025-08-21
The orders follow a petition filed by Nakuru-based surgeon Dr Magare Gikenyi, alongside Eliud Karanja Matindi, Philemon Abuga Nyakundi, and Dishon Keroti Mogire.  
Senate to hear governor Mutai's impeachment in plenary next week  
Date: 2025-08-20
Eric Mutai The Senate will handle the impeachment in a full House session, in line with Section 33A of the County Governments Act and Senate Standing Order 81B(2).  
Search results 1 until 10 of 1573