Skip to main content Skip to page footer

Ufunguzi wa kituo cha upasuaji Utange afueni kwa wakazi

Gavana Nassir alisema Hospitali hiyo ya kiwango cha Level 4 itakuwa ya kwanza kushughulikia upasuaji wa tatizo la kupasuka midomo kwa watoto wachanga.

Utange

Gavana wa Mombasa Abdulswamad Sheriff Nassir (kati) akijionea ndani ya Hospitali ya Kisasa ya Upasuaji iliyoko Utange, Mombasa. Picha/Mishi Gongo

Sekta ya afya katika Kaunti ya Mombasa imepigwa jeki baada ya kaunti hiyo kufungua kituo cha upasuaji katika eneo la Utange eneobunge la Kisauni.

Ufunguzi huo utasaidia pakubwa kupunguza msongamano wa wagonjwa wanaohitaji upasuaji katika Hospitali Kuu ya Rufaa Makadara.

Aidha itapunguza hatua ambayo wakazi walilazimika kusafiri ili kupata huduma za upasuaji.

Ufunguzi wa kituo hicho uliongozwa na gavana wa Mombasa Abdulswamad Sheriff Nassir, afisa mkuu wa hospitali ya Makadara Dkt Iqbal Khandwalla na viongozi wengine katika serikali ya kaunti ya Mombasa.

Khandwalla alisema kituo hicho kitasaidia pakubwa katika kupunguza msongamano na kutoa matibabu kwa muda ufaao.

Bi Mary Wambo, mmojawapo wa wazazi na ambaye mtoto wake alufanyiwa upasuaji baada ya ufunguzi wa kituo hicho, alieleza kuwa kituo hicho kimetoa afueni si kwa wazazi wenye watoto waliopasuka midomo tu bali hata wakazi watakaohitaji upasuaji aina nyingine.

"Kumekuwa na shida ya watu kupanga foleni katika hospitali kuu ya maji wa Mombasa kutafuta huduma za upasuaji.Wengi wamekuwa wakiumia kwa kukosa kutibiwa kwa muda unaofaa,kituo hicho kitasaidia kupunguza msongamano,"akasema.

Gavana Nassir alisema Hospitali hiyo ya kiwango cha Level 4 itakuwa ya kwanza kushughulikia upasuaji wa tatizo la kupasuka midomo kwa watoto wachanga.

“Kuanzia kaunti ya Kilifi hadi Mombasa hakuna hospitali ya umma inayoweza kufanya upasuaji huu hii itakuwa ya kwanza,Tumeianzisha ili kuwasaidia watoto waliopaasuka midomo," alisema.

Gavana pia alisema kaunti ya Mombasa ina mpango wa kutoa matibabu bila malipo kwa watoto chini ya umri wa miaka mitano licha ya mabadiliko ya bima mpya ya afya kutoka NHIF hadi SHA akiagiza maafisa husika kulifanikisha hilo katika hospitali zote za umma.

“Tulikuwa na mpango kila mtoto wa chini ya miaka mitano atibiwe bure katika hospitali za kaunti. Nadhani baada ya kuingia hii mambo ya SHA na SHIF kukawa na mchanganyiko wafanyakazi wa kaunti hakuweza kuelewa, sasa yale nimesema iweze kueleweka waziwazi hakuna mtoto yeyote wa chini ya miaka 5 ambaye ni wa Mombasa anastahili mzazi wake kulipishwa hata peni katika taasisi zetu za afya za kaunti.” Akasema.

Nassir pia alisema serikali yake ikishirikiana na wawakilishi Wadi na maafisa wa afya wa nyanjani na viongozi wengine watafanya zoezi la usajili wa bima mpya ya afya ya SHA kwa wakazi wa Mombasa akisema serikali hiyo aidha itawalipia wasiojiweza.

mombasa
1573 results:
Raila takes holiday abroad, sparks debate online  
Date: 2025-08-24
Raila Odinga His retreat, though brief, arrives at a moment when speculation on succession politics and strategic maneuvering is high.  
End of the road for East Africa as hosts crash out of CHAN 2024  
Date: 2025-08-24
Senegal's Seyni Ndiaye shoots the ball past Ugandan player during their CHAN 2024 quarter-final match The East African dream is over--at least for now--and the Pamoja nations are left with memories of vibrant crowds, carnival atmospheres, and fleeting hope.  
Kenya vs Madagascar: Harambee Stars bow out of CHAN after penalty nightmare  
Date: 2025-08-23
Kenya Squad The match remained deadlocked through extra time, prompting a dramatic penalty shootout.  
East Africa’s hopes rest on Uganda as Kenya and Tanzania crash out of CHAN  
Date: 2025-08-23
Uganda Cranes The Cranes face Senegal in Kampala on Saturday (today) for a place in the last four(4).  
UoN pharmacy alumni mark golden jubilee with free medical camp  
Date: 2025-08-23
golden jubilee medical camp During the medical camp event, the Pharmaceutical Society of Kenya (PSK) raised alarm over rising cases of unqualified individuals infiltrating pharmacies.  
CHAN Quarter-Finals Set: Stakes high for hosts and challengers alike  
Date: 2025-08-22
Benni McCarthy Kenya, who topped Group A with 10 points, are under intense pressure to deliver in front of their home fans and reach the semi-finals for the first time.  
Speaker Wetang'ula warns MPs against corruption, absenteeism  
Date: 2025-08-21
Moses Wetang'ula The Speaker addressed claims of legislators soliciting inducements to influence legislation.  
Gachagua returns from a six-week US tour amid chaos at Kamukunji rally  
Date: 2025-08-21
Rigathi Gachagua The turbulence marked a dramatic contrast to the peaceful and symbolic nature of his US mission.  
High Court halts Ruto’s anti-corruption taskforce  
Date: 2025-08-21
The orders follow a petition filed by Nakuru-based surgeon Dr Magare Gikenyi, alongside Eliud Karanja Matindi, Philemon Abuga Nyakundi, and Dishon Keroti Mogire.  
Senate to hear governor Mutai's impeachment in plenary next week  
Date: 2025-08-20
Eric Mutai The Senate will handle the impeachment in a full House session, in line with Section 33A of the County Governments Act and Senate Standing Order 81B(2).  
Search results 1 until 10 of 1573