Skip to main content Skip to page footer

Wanafunzi wa Kayole One wanufaika na mpango wa usalama barabarani

Barabara zinatengenezwa kuwa salama katika mpango unaoleta pamoja Wakfu wa FIA, Halmashauri ya Barabara za Mijini Nchini (KURA) na mashirika mengine.

Picha ya pamoja ya Mkurugenzi wa Mipango katika Wakfu wa FIA Bi Agnieszka Krasnolucka akiwa na maafisa wa trafiki na wenzao wa Barabara za Mijini (KURA), walipotoa mafunzo kuhusu usalama barabarani. Picha/AVDelta News

Wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Kayole One, eneo la Embakasi ya Kati wamenufaika na mradi wa Safari Salama na Afya hadi Shuleni, unaolenga kupunguza ajali barabarani baada ya Wakfu wa FIA kwa ushirikiano na Halmashauri ya Barabara za Mijini Nchini (KURA) na mashirika mengine kuunda barabara zenye alama.

Hii ni kufuatia visa vya kuhuzunisha ambapo wanafunzi wanne walipoteza maisha yao kwenye barabara ya Kayole One karibu na makutano na barabara ya Spine.

Barabara hiyo iliwekwa njia ya miguu, na vivuko vya pundamilia ili kupunguza ajali. Itasaidia wanafunzi 3,800.

Mhadisi wa KURA Isaac Gitoho alisema ujenzi huo wa barabara hiyo iliyowekwa alama mbalimbali ulilenga kupunguza vifo ambavyo husababishwa na wenye pikipiki na magari.

“Vifo hivi hutokea kwa sababu hakuna nafasi ya kutumia kwa waendao kwa miguu. Ukiangalia hii shule, wanafunzi ni wengi na wanatumia hii barabara,” alisema Bw Gitoho.

Mkurugenzi wa Mipango katika Wakfu wa FIA Agnieszka Krasnolucka, alisema watoto huathiriwa punde tu ongezeko la magari linaposhuhudiwa. Bi Krasnolucka alisema barabara hiyo ya umbali wa mita 400 za njia ya kutembea, iligharimu Sh3.2 milioni kufanywa ya kisasa.

“Huu ni mradi unaolenga shule nyingi Barani Afrika. Lengo letu ni kuhakikisha maafa haya hayatokei tena siku zijazo. Katika wiki chache zilizopita, tumekuwa tukihamasisha wanafunzi umuhimu wa hatua za usalama zilizowekwa karibu na shule,” alisema Bi Krasnolucka.

Mkurugenzi wa Shirika la Amend nchini Tanzania na Afrika Bw Simon Kalolo alisema waathiriwa wengi wa ajali wanaotumia miguu ni wa umri kati ya miaka mitano(5) hadi 29.  Alisema mradi huo utatekelezwa katika miji zaidi ya 10 katika nchi 10 Barani Afrika.

“Hapa tumejenga zaidi ya mita 400 za njia za watembeao kwa miguu zenye upana wa zaidi ya mita mbili(2), kutoa nafasi salama kwa watoto, watumiaji wa viti vya magurudumu, na wanaotembea kwa miguu wengine,” Bw Kalolo alisema.

Katika ripoti ya Mamlaka ya Usafiri na Usalama Barabarani (NTSA) 2024, inaonyesha kuwa watoto 424 wenye umri wa miaka kati ya mitano(5) hadi 19 walihusika kwenye ajali za barabarani.

1573 results:
Raila takes holiday abroad, sparks debate online  
Date: 2025-08-24
Raila Odinga His retreat, though brief, arrives at a moment when speculation on succession politics and strategic maneuvering is high.  
End of the road for East Africa as hosts crash out of CHAN 2024  
Date: 2025-08-24
Senegal's Seyni Ndiaye shoots the ball past Ugandan player during their CHAN 2024 quarter-final match The East African dream is over--at least for now--and the Pamoja nations are left with memories of vibrant crowds, carnival atmospheres, and fleeting hope.  
Kenya vs Madagascar: Harambee Stars bow out of CHAN after penalty nightmare  
Date: 2025-08-23
Kenya Squad The match remained deadlocked through extra time, prompting a dramatic penalty shootout.  
East Africa’s hopes rest on Uganda as Kenya and Tanzania crash out of CHAN  
Date: 2025-08-23
Uganda Cranes The Cranes face Senegal in Kampala on Saturday (today) for a place in the last four(4).  
UoN pharmacy alumni mark golden jubilee with free medical camp  
Date: 2025-08-23
golden jubilee medical camp During the medical camp event, the Pharmaceutical Society of Kenya (PSK) raised alarm over rising cases of unqualified individuals infiltrating pharmacies.  
CHAN Quarter-Finals Set: Stakes high for hosts and challengers alike  
Date: 2025-08-22
Benni McCarthy Kenya, who topped Group A with 10 points, are under intense pressure to deliver in front of their home fans and reach the semi-finals for the first time.  
Speaker Wetang'ula warns MPs against corruption, absenteeism  
Date: 2025-08-21
Moses Wetang'ula The Speaker addressed claims of legislators soliciting inducements to influence legislation.  
Gachagua returns from a six-week US tour amid chaos at Kamukunji rally  
Date: 2025-08-21
Rigathi Gachagua The turbulence marked a dramatic contrast to the peaceful and symbolic nature of his US mission.  
High Court halts Ruto’s anti-corruption taskforce  
Date: 2025-08-21
The orders follow a petition filed by Nakuru-based surgeon Dr Magare Gikenyi, alongside Eliud Karanja Matindi, Philemon Abuga Nyakundi, and Dishon Keroti Mogire.  
Senate to hear governor Mutai's impeachment in plenary next week  
Date: 2025-08-20
Eric Mutai The Senate will handle the impeachment in a full House session, in line with Section 33A of the County Governments Act and Senate Standing Order 81B(2).  
Search results 1 until 10 of 1573